KILIMO CHA MKONGE
MUWASILISHAJI; MBARAKA BATARE
KUTOKA; KITUO CHA UTAFITI WA KILIMO
MLINGANO
IDARA YA MKONGE
SLP 5088 TANGA TANZANIA
PHONE; 0717698998/0769323117
UTANGULIZI
KWA UJUMLA KUHUSU ARI MLINGANO
Kituo
cha Utafiti Mlingano ni kituo cha serikali kikonge kilichoanziswa mwaka 1934
kikiwa na idara moja ya mkonge mpaka sasa kinajiusisha na utafiti katika idara
kuu tatu utafiti wa mkonge, rutuba ya udongo (soil fertility) na asilimali
ardhi (land survey) ili kuiweza jamii ya watanzania Kulima kwa tija na kupata
mazao bora na mengi ili kuendeleza vipato vyao kwa mmoja mmoja na kwa taifa pia
KILIMO CHA MKONGE TANZANIA
UTANGULIZI WA ZAO LA MKONGE
Zao
la mkonge liliingizwa nchini mwaka 1892 na mtaalamu wa kijerumani Dr. Richard
Hindorff ambaye alikuwa ni mtafiti wa mimea na udongo. Mtaalamu huyo alichukua
miche 1000 kutoka pwani ya Mexico kwenye jimbo la Yuctan ambalo ambalo ndilo
asili ya jina katani na kuisafisha kwa magendo kwa kupitia Frolida , Marekani
na Humburg Ujerumani. Kati ya miche 1000, ni miche 62 tu ndiyo iliyofika
Tanganyika na ilipandwa sehemu iitwayo kikokwe huko Pangani Tanga. Mkonge
ulisambaa maeneo mengi ya Tanganyika mpaka kufikia mwanzoni mwa miaka 1960 Tanganyika ilikuwa inaongoza kwa
uzalishaji wa mkonge ikifatiwa na Brazil na mexico kwa mauzo ya tani 230,000
kwa mwaka nje ya nchi . Kutokana na sababu mbalimbali zilizo jitokeza miaka ya
1970 uzalishaji ulipungua toka tani 230,000 hadi tani 19,700 kwa mwaka 1997.
Hata ivyo mageuzi ya kiuchumi yaliyoanza miaka 1980 ambayo yalilenga katika
ubinafisishaji na biashara huria , uhuru wa taasisi za kifedha za ndani na nje
ya nchi yalifufua kilimo cha mkonge na hasa kukamilika kwa ubinafishaji mwaka
2005 uzalishaji umepanda hadi kufikia tani 40,000 mwaka 2015 hii inatokana na
kuongezeka kwa mahitaji ya mkonge na bidhaa zake pamoja na kupanda bei kwenye
soko la dunia pamoja na ndani. Soko kuu la mkonge wa Tanzania ni china, Saudi
Arabia , India, Uhispania, Ujerumani, Uingereza, Kenya, Uganda na Nigeria.
KWANINI ZAO LA MKONGE
Kutokana
na mabadiliko makubwa ya hali ya hewa kwa sasa wakulima wengi wamekuwa wakikosa
mavuno kutokana na kutegemea mvua ambazo kwa sasa mtiririko wake siyo mzuri
ivyo wataafiti wa mkonge tunahamasisha kilimo cha kilimo cha mkonge kwa
wakulima wadogo nchi nzima ili zao litumike katika kuwaongezea wananchi kipato
kutokana na sifa za mkonge kama zifuatazo;
i)
Zao la mkonge linavumilia sana ukame
ii)
Ni zao ambalo halina msimu maalumu wa
kupanda hivyo kupelekea kuweza kupandwa wakati wowote na pia halina wakati
maalumu wa kuvunwa pale linapokuwa tayari kuvunwa
iii)
Zao la mkonge linaweza kuchanganywa na
mazao mengine ya msimu kama kunde, mahindi, maharage , alizeti, njegere na
karanga.
iv)
Ni zao ambalo halina uhaba wa vipando.
v)
Bidhaa zitokanazo na mkonge zinaweza
kutumika katika tasnia ya kilimo, nishati, ujenzi, famasia, magari, meli,
majumbani,ofisini na mazingira
vi)
Mmea wa mkonge unaweza kuishi kwa
kipindi cha miaka 10-25 hivyo kumuhakikishia mkulima kipato cha uhakika
vii)
Mkonge ni
zao linalo staimil magonjwa, wadudu
na maguu na hata upungufu wa rutuba
kwenye udongo.
UZALISHAJI WA MKONGE
Kilimo
bora cha zao la mkonge ni muhimu ili kuongeza tija kwa mkulima . kumbukumbu
tulizonazo ni kwamba wenzetu Uchina wanavuna tani 4-5 kwa hekta kwa kuboresha
kilimo hicho ukilinganisha na tani 1-2
kwa hecta hapa Tanzania. Ivyo ni muhimu tuboreshe kilimo chetu ili tuweze
kupata mavuno mengi na kwa hiyo kushindana na wenzetu kwenye soko la kimataifa.
Mambo yafuatayo ni yakuzingatia katika uzalishaji wa mkonge;
i)
Maandalizi ya miche bora ya mkonge
ii)
Utunzaji wa vitalu vya mkonge
iii)
Upandaji
wa mkonge shambani
iv)
Utunzaji wa mkonge shambani
v)
Kilimo mseto cha mkonge na mazao mengine
yachakula
i)
MAANDALIZI
YA VITALU VYA MKONGE
Uchaguzi
sahihi wa miche ya mkonge na maadalizi ya mazuri ya kitalu kwa ajili ya
upandaji wa miche ya mkonge ni muhimu kwa ukuaji haraka na hatimaye utoaji wa
mavuno bora na mengi ya zao la mkonge.
Kuna
aina nne ya vipando vya mkonge;
·
Vikonyo
(bulbils) huota kwenye mlingoti baada ya maua ya mkonge kupukutika
·
Machipukizi (suckers) huchipua kutoka kwenye
mmea wa mkonge
·
Miche inayozalishwe ndani ya maabara kwa
njia ya tissue culture (mtc lab)
·
Miche inayotokana na mizizi au tumba za
mkonge huitwa rhizomes japo aina hii ya miche sasa hivi haitumiki sana hapa
nchini.
ii)
Utunzaji wa vitalu vya mkonge
·
Palizi –upaliliaji kwa jembe la mkono
kwa kawaida palizi linaweza kufanyika mara 4-8 kutegemea na udongo.
-
Upaliliaji kwa kutumia dawa za magugu
mfano hy-varax hutumika sana kuzuia magugu katika bustani za mkonge huzuia
uotaji wa magugu kwa muda wa miezi sita mfululizo ambayo utumika kwa kiasi cha
kilo 4.5/ha nah ii dawa inashauriwa inyunyiziwe bustanini wakati udongo una
unyevunyevu.
·
Namna ya kurutubisha vitalu
-
Taka za mkonge ( sisal waste)
-
Mbolea ya chunvichunvi zenye kirutubisho
cha nitrogen 30kg /ha kama CAN, SA, and
UREA kwa kukuzia
-
Mbolea aina ya potash kama MOP na DAP
-
Wadudu na magonjwa ya mkonge kama tembo
wa mkonge ( sisal weevil) na scale na
magonjwa kama kuoza kwa mashina (bole rot) , ugonjwa wa pundamilia (zebra leaf
rot) na ugonjwa wa mabaka kwenye majani (korogwe leaf sport)
iii)
UPANDAJI
WA MKONGE SHAMBANI
·
Uchaguzi na upandaji wa miche ya kupanda
(grading) ukubwa wa miche ya kupanda ni bora iwe na urefu kati ya sentimita
50-70 na uzito kati ya kilo 2-4 miche ipangwe katika madaraja kufuatana na
ukubwa
-
Uchimbaji wa miche huchimbwa kwa kutumia
jembe au sululu ili kitunguu (bole)
kisikatwe ili kuepusha kushambuliwa na wadudu.
-
Kutayarisha miche kwa kukata mizizi bila
kuaribu shina na majani yaliyonyauka yaondolewe
-
Upandaji wa kutumia machipukizi
(suckers) ikusanywe kutoka katika mashamba yenye mkonge mdogo si zaidi ya
mikato 2
-
Kuligawa shamba katika maboma kwa ajili
ya kupanda mkonge shambani
·
Mifumo ya kupanda mkonge shambani
-
Mstari mmoja (single row) kwa nafasi ya
3.5 x 0.75 mita
-
Upandaji wa mistari miwili (double row )
upandaji huu miraba miwili huwekwa karibu ili kutoa nafasi pana kati ya miraba
hiyo. Nafasi ya upandaji utegemea aina ya mkonge
Ø Mkonge aina ya sisalana
nafasi pana ni mita 3.5 na nafasi kati ya mistari miwili iliyo karibu ni mita 1
wakati nafasi kati ya mmea mmoja na mwingine ni setimita 90 (3.5 +1 x 0.9)
mita. Hutoa mimea 5,000 kwa hekta.
Ø Mkonge
chotara (H.11648) nafasi pana ni mita 4 na nafasi kati ya mistari iliyo karibu
ni 1 pia nafasi kati ya mmea mmoja na
mwingine ni mita 1 (4 +1 x 1) mita. Upandaji huu utoa mimea 4,000 kwa hekta.
·
Muda wa kupanda inashauriwa kupanda
mkonge kabla mvua hazijaanza na mkonge upandwe kina cha sentimita 8 ardhini na
kushindiliwa
iv)
UTUNZAJI
WA MKONGE SHAMBANI
Ili mkulima wa mkonge
apate mavuno mengi ni vyema kuzingatia yafuatayo
- Matumizi
ya taka za mkonge (sisal waste) ili kuifadhi unyevunyevu na kurutubisha udongo.
- Matumizi
ya chokaa (agriculture lime) ili kuongeza chachu pH mpaka 5.5-5.8 inayotakiwa
na mkonge.
- Kuweka
mbolea za chunvichunvi zenye kirutubisha cha nitrogeni mfano CAN UREA,
potasiam na phosphorus kama MOP, TSP NA
DAP.
-
Udhibiti wa magugu ili kuepusha kutumia
maji na virutubisho vinavyotakiwa kutumiwa na mmea. Kwakutumia njia zifuatazo;-
kutumia jembe au nyengo, kutumia madawa mfano bromacil, kutumia jamii ya
mikunde (cover crop) mfano tropical kudzu.
v)
KILIMO
MSETO CHA MKONGE NA MAZAO MENGINE YA CHAKULA
Eneo
linalotumiwa kwa mkonge ni asilimia 60 na kiasi kilichosalia asilimia 40 hubaki
tupu ivyo ni bora Kulima na mazao mengine faida za Kilimo mseto
-
Kutumia ardhi kwa ufanisi
-
Kuzalisha mazao Zaidi ya moja katika
eneo hilo na kwa Gharama ndogo.
-
Kwa kupanda mazao jamii ya kunde
husaidia kuongeza rutuba ya udongo.
-
Kupata Chakula hasa kwa wakulima wadogo na
kwa mazao yanayofunika ardhi na kupunguza mmomonyoko wa ardhi kwa njia ya upepo
na maji.
·
Mazao yanayofaa kuchanganywa na mkonge
maharage, kunde, karanga, soya, choroko alizeti, ufuta, mahindi nk
·
Mazao yasiyofaa kuchanganywa na mkonge
ni mazao ya kudumu kama migomba, minazi, mikorosho na michungwa mtama uwele viazi vitamu na mihogo
2. UVUNAJI WA MKONGE
i)
Ukataji wa mkonge ili kupata singe
mkonge uvunwa majani kwa kuzingatia yafuatayo
-
Jani linalovunwa ni lazima liwe na urefu
unaozidi sentimeta 90
-
Ni lazima jani liwe na mwanguko usiozidi
digrii 45%
-
Ni lazima likatwe kwenye shingo yake
-
Ni marufuku kukata kitunguu au mape
ii)
Usombaji wa majani yaliyokatwa
iii)
Usindikaji
iv)
Kulainisha singa (brushing)
v)
Kufunga mizingo kwenye press (pressing
machine)
vi)
Kupanga madaraja ya singa (grading) kwa
kuangalia urefu wa singa narangi ya singa
IMEANDALIWA
NA; MR. MBARAKA BATARE
MUTAFITI
WA MKONGE
ARI-MLINGANO
TANGA TANZANI
SIMU;
0769323117/0717698998
nimeipenda mimi ntemange bujiku namba yangu ni 0763099028 na barua pepe ni ntemangeb@gmail.com naomba ushauri niko shinyanga
JibuFutaNimeipenda ubarikiwe sana, mimi naitwa Yassin Manota, nipo morogoro nataka nipande katani hekar 20. Namba yangu ya sim ni 0756463833 na mail yangu ni yassnota@gmail.com naomba nisaidie soft copy ya makala hii na nyingi kama zipo kwa sisi tunaoanza.
JibuFutaHongera kwa kutupa darasa,ubarikiwe sana,vipi kuhusu masoko na bei ya mkonge kiongozi!
JibuFutaluka
FutaAsante kwa darasa.nauliza mkoani ruvuma wilaya ya mbinga mikonge inastawi?
JibuFutaFUMBA HAMADI
FutaAsante sana kwa kutupa darasa kwa sisi tunaoanza kilimo hiki cha Mkonge.
JibuFutaShukura sana Kwa elimu juu ya zao LA mkonge.
JibuFutaNAHITAJI MBEGU BORA ZA MKONGE NAPATAJE? MIMI NIKO SINGIDA VIJIJINI KWA NAMBA 0752795267
JibuFutaNaomba maelekezo zaidi namna ya kulima zao hili, nipo Kigoma
JibuFutaUoande wa gharama na faida kwenye uwekezaji wa mkonge ni zipi kwa hekari 1
JibuFutaHekari kumi10 za mkonge Kwa sasa zaweza kutoa tani ngapi pia naweza kuuza Kwa bei gani?. Naombeni mnijuze.
JibuFutaNilitaka kujua zao la mionge linachukua muda gani toka kupanda mpaka kuanza kuvuna especially kwa mbegu ya chotara???
JibuFutaMiaka 3 ndio unaanza kuvuna
FutaNa mkulima anaweza kupata faida kiasi gani kwa hekari moja ambayo imehudumiwa vizuri??!
JibuFutaNimefatilia vzr kipindi cha tari mkonge
JibuFutaNimeupenda , niko tabora nataka mbegu bora za muda mfupi zinauzwa bei gani maana namuona waziri mkuu kassim kahamasisha kweli nami nimependa , nipo tabora mjini ninahekali 2 nata nipande mkonge naomba mbegu nizipate , namba zangu ni
0689997575
0769368615
Nielimu nizuli san tunakushukur san mtalam
JibuFutaNimependa maeleozo yako
JibuFutaNitumie makala hii kupitia
JibuFutarashidntolok@gmail.com
Nimejifunza Kitu
JibuFutaAhsante
JibuFutaHii ni mada nzuri sana kwa maendeleo ya kilimo na kupunguza umaskini wa mkulima
JibuFutaMaelezo yako ya kitaalamu yanahamasisha sana na kututia moyo wa kushiriki katika kulifufua zao la Mkonge, kwa manufaa yetu na Taifa kwa ujumla. Binafisi ninalo eneo kama ekari 20 ningependa nilime zao hilo kwa kutumia mbegu mpya za " Hybrid " je utaratibu wenu wa kuzipata ukoje? Mob: 0782 780389 ( Msuwakollo)
JibuFutaMaelezo yako ya kitaalamu yanahamasisha sana na kututia moyo wa kushiriki katika kulifufua zao la Mkonge, kwa manufaa yetu na Taifa kwa ujumla. Binafisi ninalo eneo kama ekari 20 ningependa nilime zao hilo kwa kutumia mbegu mpya za " Hybrid " je utaratibu wenu wa kuzipata ukoje? Mob: 0782 780389 ( Msuwakollo)
JibuFutaMaelezo yako ya kitaalamu yanahamasisha sana na kututia moyo wa kushiriki katika kulifufua zao la Mkonge, kwa manufaa yetu na Taifa kwa ujumla. Binafisi ninalo eneo kama ekari 20 ningependa nilime zao hilo kwa kutumia mbegu mpya za " Hybrid " je utaratibu wenu wa kuzipata ukoje? Mob: 0782 780389 ( Msuwakollo)
JibuFutaMimi Ntemange Bujiku ninaipenda biashara ya mkonge lakini nashindwa kuzipata mbegu za mkonge naomba nisaidiwe Niko kishapu shy
JibuFutaKwanamba 0763099028 napatikana
JibuFutaEbu nieleweshe vizuri kwenye nafasi za kupandia
JibuFutaCasino - Mapyro
JibuFutaCasino Hotel Map and reviews. Casino 논산 출장마사지 Resort, 경산 출장안마 Laughlin. Phone Number, 1-800-522-4700. Hours, Mon-Fri 9:00 am - 계룡 출장마사지 9:00 pm. Directions, 김제 출장안마 1-888-522-4700. Casino Address, 777 Casino Parkway. Map 남원 출장샵